Damien Soul
Damien Soul na Joh Makini
Yule nguli wa muziki wa Bongo Fleva hapa nchini aliyewahi kutamba na kibao cha Hakuna Matata, pamoja na kushiriki katika shindano kubwa Afrika ya Mashariki, yaani Tusker Project Fame, Damien Soul, hivi karibuni alizungumza moja kwa ,moja na Blog hii, kuwa yuko mbioni kufyetua kibao chake kikali alichokibatiza jina la Ni Penzi, na kusema kuwa ndani yake yumo mweusi Joh Makini, aliyefanya yake kuitia nakshi ngoma hii.
Aidha katika kuizungumzia background ya msanii huyu kimuziki, twaweza sema ni moja kati ya vijana wachache waliyowahi kufanya mengi katika tasnia hii na kuwa ni moja kati ya wanaoshiriki matamasha ya Sauti za Busara, kule kwenye visiwa vya karafuu, Zanzibar. Kila la kheri kwake!
0 comments:
Post a Comment