Decoration & Catering Services

Decoration & Catering Services

Boutique

Boutique

Sunday, December 1, 2013

Hoja ya kumwondoa Waziri Mkuu Somalia

 Waziri Mkuu wa Somalia Abdi Farah Shirdon

Bunge la Somalia limeanza kujadili hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu wa nchi hiyo Abdi Farah Shirdon ambaye amekuwa haelewani na rais wa nchi hiyo Hassan Sheikh Mahamud.

Bwana Shirdon hivi karibuni amekuwa akimkosoa rais wa nchi hiyo kwamba amekuwa akiongoza nchini hiyo bila kufuata katiba.

Wafuasi wa rais Hassan wanasema Waziri Mkuu huyo ameshindwa kutekeleza majukumu yake na uongozi wake umekuwa hauna mafanikio.

Waandishi wa habari waliyopo Somalia wanasema mgawanyiko katika serikali ya Somalia iliyoundwa mwaka jana, unatishia juhudi za kuimarisha utulivu nchini humo baada ya nchi hiyo kuathirika na mgogoro kwa takrabani miongo miwili.

0 comments:

Post a Comment