Decoration & Catering Services

Decoration & Catering Services

Boutique

Boutique

Sunday, December 1, 2013

Ghasia za kisiasa zaitingisha Bangkok

Polisi ya Thailand imetumia gesi ya kutowa machozi na maji ya kuwasha kuwatawanya waandamanaji Jumapili(01.12.2013) wakati walipokuwa wakijaribu kuvamia makao makuu ya serikali kumpinduwa Waziri Mkuu Yingluck Shinawatra.
Maandamano ya kupinga serikali Bangkok (01.12.2013)

Ghasia hizo ni mfulululizo wa mfarakano wa kiraia katika nchi hiyo ya kifalme tokea magenarali wenye kuupendelea ufalme kumpinduwa tajiri mkubwa wa nchi hiyo aliekuja kuwa waziri mkuu Thaksin Shinawatra miaka saba iliopita.

Maandamano hayo ya mitaani yenye lengo la kuindowa serikali ya Yingluck na badala yake kuliweka "baraza la wananchi " lisilochaguliwa na wananchi ni maandamano makubwa kabisa ya umma kuwahi kushuhudiwa tokea maandamano ya kumuunga mkono Thaksin mjini Bangkok miaka mitatu iliopita kusababisha kuuwawa kwa watu chungu nzima kutokana na maandamano hayo kuvunjwa kwa nguvu na jeshi.

0 comments:

Post a Comment