Decoration & Catering Services

Decoration & Catering Services

Boutique

Boutique

Monday, December 30, 2013

KIMATAIFA: Bangui hali yazidi kuwa mbaya.



Shirika la msalaba mwekundu limesema limegunduwa maiti zipatazo 40 katika mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika kati Bangui.
Kufuatia hali hiyo, Marekani imesema inawasiwasi wa kuzuka kwa mapigano mapya katika taifa hilo la kiafrika.
Kugunduliwa kwa maito hizo, kunakuja baada ya mapigano wakati zaidi ya watu elfu moja wakiwa wameuwawa katika mapigano ya wiki tatu baina ya Wakristo na waislamu.
Taarifa kutoka Shirika la habari la AFP zinasema kuwa miongoni mwa waliouawa, ni walinzi watano wa amani kutoka Chad,ambao walishambuliwa na wanamgambo wa Kikristo, wajulikanao kama 'anti-balaka' katika mji mkuu, Bangui, siku ya Jumatano.
Kufuatia kuzuka kwa mapigano hayo juzi, kulizusha hali ya wasi wasi miongoni mwa maelfu ya wakaazi wa mji wa Bangui ambao walilzamika kukimbilia katika eneo la Uwanja wa Ndege kwa ajili ya kupata hifadhi na vyakula, eneo ambalo walinda amani kutoka Ufaransa na Afrika wamepiga kambi.

0 comments:

Post a Comment