Decoration & Catering Services

Decoration & Catering Services

Boutique

Boutique

Friday, April 25, 2014

Je, kuporomoka kwa afya ya 'Baghdad' wa 'Mexicana La cavela' ni kwa mazoezi tu?




Pichani; Baghdad wa Mexicana La cavela alivo sasa.

Katika pitapita zangu za hapa mjini, jana nikakutana na rappa wa Kibongo aliyekuwa akichipukia vyema sana katika muziki huu wa Bongo Fleva, Baghdad wa Mexicana Lakavela. 

Mimi nilibahatika kumjua kijana huyu hata kabla ya kuvuma sana kwenye game, tulipokuwa twasoma nae shule moja, pale Azania Secondary school 2007-2009, mimi nikiwa natumia lebo ya bluu nae nyekundu.

Sasa kilichonisukuma mpaka saa hii nimeamua kuipandisha stori yake kwenye mtandao huu;  ni mabadiliko makubwa sana ya kimuonekano na kiafya ya Baghdad, ambae pia alikuwa ni mahiri sana kwa kucheza Basketball shuleni kwetu.
 Katika moja ya pozi akiwa na afya yake ya awali.

Sio siri kijana huyu amebadilika sana, mpaka ninaogopa kila niikumbukapo picha yake ya Azania na hii ya jana niliyomuona tena live baada ya miaka minne.

Hiyo jana sasa nilipokutana nae nilimsalimia kama mtu nisiye mjua  ila kwa ukarimu na nilipo jaribu kumuuliza mambo fulani fulani ya huko nilikokuwa naenda, aliniambia ndiko pia aendako na tena ni Mwenyeji. Na kwa bahati nzuri sana akaniambia kuwa sura yangu si ngeni kwake.


Kwa upande wangu nilifurahi kusikia hivyo huku moyoni nikijua kile nilichokuwa nakitafuta nitakipata kiurahisi maana nishampata mtu anaenifahamu. 

Baghdad akiwa kwa stage.


Baada ya hatua chache mbele bro wangu huyu wa xul akaamua kujitambulisha kuwa yeye ni Baghdad. Ebwana siyo siri nilishtuka sana na kumuuliza yeye ni Baghdad yupi wa Azaboy au yupi na mbona kakonda sana?( Mungu anisamehe tu).  Ndipo rappa huyu alipo nijibu kuwa ndiye huyo huyo wa Azaboy na kuwa ni mazoezi tu ndiyo yaliyo mpunguza. 

Lakini hakuonekana kuwa na ujasiri tena, akaamua kuniacha mapokezi.


Ninachotaka kukijua toka kwenu fans wake katika muziki huu Hip hop, marafiki, ndugu na wale wote mlio karibu nae mwanamuziki huyu Je, ni kweli mshikaji anapiga mazoezi kiasi cha kupungua vile, au ana tatizo gani linalo msumbua kiasi cha kuwa alivyo sasa? 


Hebu tumia muda wako ku-comment hapo chini about this story. What’s  wrong to my brother kwa vile unavohisi na unavojua!?

0 comments:

Post a Comment